NMB:Droo ya kwanza ya Pata Patia yafanyika nchini
Washidi 24 wamejishindia fedha taslimu baada ya droo ya kwanza ya promosheni ya Pata Patia na NMB kufanyika nchini. Washindi hao wametokea mikoa mbali mbali ikiwemo Dar es Salaam, Morogoro, Mbeya na Mtwara. Promosheni ya Pata Patia ilizinduliwa mwanzoni wa mwezi Machi na zaidi ya shilling millioni mia tatu zinashindaniwa.
NMB MKWAWA: Meneja wa tawi la NMB Mkwawa kulia, Sumka Mbuba akimpongeza Andarson Lyandala baada ya kujishindia kiasi cha shilingi milioni tatu . Promosheni ya Pata Patia inayoendelea kwa wateja wa NMB inatoa nafasi kwa kila alie mteja kushiriki promosheni hii kwa kuweka fedha katika akaunti yake mara mara .Hafla hii ilifanyika mwishoni mwa wiki Mkoani Iringa
NMB MBALIZI: Meneja wa NMB Kanda ya juu Badru Idd akimpongeza Angetile Gwakisa ambae ni mteja wa NMB kupitia tawi la NMB Mbalizi ameibuka kua mshindi wa Pata Patia kwa kujinyakulia kitita cha shilingi milioni tatu. Promosheni ya Pata Patia inayoendelea kwa wateja wa NMB inatoa nafasi kwa kila alie mteja kushiriki promosheni hii kwa kuweka fedha katika akaunti yake mara mara .Hafla hii ilifanyika mwishoni mwa wiki mkoani Mbeya
NMB Morogoro: Mshindi wa shindano la kubahatisha la Pata Patia liloandaliwa na NMB tawi la Ifakara, Agripina Liampawe akipongezwa na afisa wa benki Asha Mlawa baada ya kujishindia kitita cha shilingi milioni mbili. Promosheni ya Patapatia inayoendelea kwa wateja wa NMB inatoa nafasi kwa kila alie mteja kushiriki promosheni hii kwa kuweka fedha katika akaunti yake mara mara .Hafla hii ilifanyika mwishoni mwa wiki Mkoa wa Morogoro
NMB Sinza Dar es salaam:Meneja Kituo cha Biashara cha Benki ya NMB Sinza, Mnkande Zawadi (kushoto) akimkabidhi Bi. Devota Lihambalimo shs laki moja
NMB Sinza Dar es salaam; Nusura Mohamed ambaye ni mwalimu wa Sekondari Zinga ya Bagamoyo akipokea shs milioni moja baada ya kushinda pata patia.