BAADA ya hivi karibuni Kocha Mkuu wa Simba, Mbelgiji, Patrick Aussems kufanikiwa kuiona pacha ya mabeki wake wawili wa kati, Mganda, Juuko Murshid pamoja na Pascal Wawa, raia wa Ivory Coast, sasa ameanza mchakato wa kutaka kuiona pacha nyingine ya Juuko na Erasto Nyoni.
Aussems anataka kuiona pacha hiyo ili aweze kuamua ni pacha gani ambayo inastahili kuwa katika kikosi chake cha kwanza kwa ajili ya michuano ya Ligi Kuu Bara lakini pia ile ya kimataifa ambayo timu hiyo itashiriki mwaka huu.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Aussems alisema kuwa kabla ya kumuona Juuko uwanjani, alikuwa akijivunia pacha ya Wawa na Nyoni.
Lakini baada ya kumuona Juuko akicheza kwa kiwango cha juu akishirikiana vyema na Wawa, alivutiwa pia na pacha hiyo na kujikuta akitamani kuiona pacha ya Juuko na Nyoni.
“Nimeijaribu pacha hiyo mazoezini na nimeona jinsi inavyocheza kizuri lakini nataka nione pia katika mechi.
“Kwa hiyo, Nyoni akimaliza adhabu yake ipo siku nitawaanzisha pamoja na Juuko ili niweze kuwaona na baada ya hapo sasa ndipo nitakapojua ni pacha gani ambayo inastahili kuwa katika kikosi changu cha kwanza,” alisema Aussems.
Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam
Comments are closed.