The House of Favourite Newspapers

Obama Aagiza Uchunguzi Ufanyike Kuhusu Tuhuma za Udukuzi Uliofanywa Urusi Kumsaidia Trump

636159438258496733-ap-2016-election-wisconsin-voting

Washington (CNN): Rais Barack Obama ameagiza uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za udukuzi zilizofanywa na nchi ya Urusi katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa Marekani uliofanyika Novemba 8 mwaka huu ambapo bwana Donald Trump wa Chama cha Republican aliibuka mshindi kwa kumbwaga mpinzani wake, Bi. Hillary Clinton.

donald-trump-president-barack-obama2-700x373

Trump na Obama.

Rais Obama ameyasema hayo jana kwenye Ikulu ya nchi hiyo ‘White House’ kufuatia ripoti iliyotolewa na Central Intelligence Agency (CIA)  ikieleza kuwa, nchi ya Urusi iliingilia mfumo wa Kompyuta wa Tume ya Uchaguzi ya Marekani unaotumika kuhesabu matokeo hivyo kuuharibu kwa lengo la kumsaidia bwana Trump kushinda uchaguzi huo ambapo inasemekana tukio kama hilo lilifanyika kwenye uchaguzi wa nchi hiyo mwaka 2008.

Viongozi wa Tume ya Uchaguzi wa nchi hiyo wamesema kuwa, endapo itabainika kuwa mfumo huo ulidukuliwa na Warusi, basi kura zote zitarudiwa kuhesabiwa upya na matokeo yatatolewa kabla ya Januari 20 ambapo bwana trump anatarajiwa kuapishwa.

obamaa

Kwa upande wa Urusi wamekanusha kuhusika na udukuzi huo huku Wizara ya Mambo ya nje ya nchi hiyo ikiitaka Marekani ithibitishe iwapo kweli walidukua mfumo wa kompyuta wa uchaguzi wa Marekani. Waziri wa Mambo ya ndani wa Urusi amesema ni mara kadhaa wamewaeleza Marekani kutoa uthibitisho lakini wameshindwa kufanya hivyo.

Siku chache kabla ya uchaguzi, Serikali ya Marekani ililaani Serikali ya Urusi kwa kudukua na kuingilia mawasiliano ya Kamati Kuu ya Chama cha Democratic (Democratic National Committee) pamoja na barua pepe za baadhi ya viongozi wa Democratic na za Hillary Clinton huku mwenyekiti wake akidukuliwa na kuondolewa kwenye mtandao wa WeakLeaks.
Kwa upande wake, Rais Mteule wa Marekani amepuuza tuhuma hizo na kukanusha kuhusu nchi ya Urusi kufanya udukuzi huo kwenye mfumo wa Uchaguzi wa Marekani.
MZEE WA MIAKA 76 ALEYETANAGAZA KUTAFUTA MKE “FULL EXLUSIVE INTERVIEW”

halotel-strip-1-1

Comments are closed.