The House of Favourite Newspapers

OKWI AMPONZA CHIRWA YANGA

Chirwa.

 

MSHAMBULIAJI wa Simba, Emmanuel Okwi, ameonekana kumuumiza kichwa straika wa Yanga, Obrey Chirwa ambapo imebainika kuwa ndiye chanzo cha Mzambia huyo kushindwa kuungana na wenzake kwenye safari ya kuelekea Shelisheli kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya St Louis.

 

Chanzo makini kutoka ndani ya Yanga kimeli­ambia Championi Jumatano kuwa Okwi ndiye aliyechangia Chirwa ashindwe kwenda Shel­isheli baada ya kulazimisha kucheza mchezo wao wa ligi kuu uliopita dhidi ya Majimaji huku akiwa na majeraha ambapo alipanga kuongeza idadi ya mabao ili kumpita Mganda huyo.

 

Okwi.

 

“Ukweli ni kwamba Okwi ndiye ambaye amechangia Chirwa kubakia hapa Dar baada ya kushindwa kwenda Shelisheli kama wen­zake ambavyo walifanya kwa sababu Chirwa alilazimisha kucheza ile mechi na Majimaji huku akiwa anaumwa.

 

“Yeye alipanga atumie mchezo ule kama sehemu ya kumzidi Okwi mabao sasa bahati mbaya ni kwamba baada ya mchezo kumal­izika lile jeraha likazidi kuwa kubwa hivyo kusababisha hadi jina lake litolewe katika wale ambao wanasafiri kuelekea nchini humo kwa ajili ya mchezo wetu.

“Hata hivyo, sasa hivi bado anatamani kupo­na haraka kwa kuwa anataka kurudi uwanjani mapema ili afunge na awe mfungaji bora wa ligi,” kilisema chanzo hicho.

 Musa Mateja, Dar es Salaam

Comments are closed.