The House of Favourite Newspapers

Omog: Yanga hii moto

0

13658691_193331527749565_1712444849_n

Wachezaji wa Yanga wakipasha kabla ya mechi.

Nicodemus Jonas na Omary Mdose

PAMOJA na kuboronga kwao kwenye michuano ya kimataifa, Kocha wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog, anaamini bado Yanga ni timu ambayo itafanya vema msimu ujao kutokana na uwepo wa Mdachi, Hans van Der Pluijm.

pic+omog

Kocha wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog.

Yanga ilianza vibaya kampeni yake ya kusaka tiketi ya kufuzu nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo katika mechi nne iliambulia moja kabla ya juzi Jumamosi kupata ushindi wa kwanza kwa kuichapa MO Bejaia ya Algeria bao 1-0.

Katika mahojiano na Championi Jumatatu kuhusu anavyoijua Yanga ya sasa chini ya Pluijm, Omog hakutaka kuwa mnafiki, badala yake alimmwagia sifa Pluijm na timu yake akidai inafanikiwa kutokana na kuwa na kocha mzuri.

“Timu kutwaa ligi mara mbili na kuchukua makombe matatu kwa pamoja siyo jambo dogo. Binafsi niwe mkweli Pluijm ni kocha mzuri sana,” alisema kocha huyo wa zamani wa Azam.

Omog anaamini takwimu hizo zinawafanya Yanga kuwa wapinzani wakuu katika msimu mpya unaoanza wikiendi hii ambapo Simba watakata utepe na Ndanda kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Yanga imefufua shangwe za mashabiki wake baada ya kupata ushindi huo wa juzi.

Msimu ujao unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa, hasa kutokana na Simba na Azam nazo kujipanga huku Yanga ikionekana kuwa na makali yaleyale.

Leave A Reply