The House of Favourite Newspapers

Oya mwana acha kumaindisha ganda la ndizi!

0

Woraa…woraaa…wooze! Oya masela wa kitaa vepe? Kipande hii mambo mzuksi… ni hatare! Welikam kwa sana kwa fasi ya jamvini kozi niliwamisi kidizaini f’lani tangu lasti wiki makachala wangu.
Mazee ishu ni nyingi kinoma na taimu inamuvu spidi mia na mbao kwenye kitu cha kona shaa… Sasa mwaka huooo…unatambaa tu mtu fedenge Ino  jicho kodoo…anasapraizi tu haelewi nini kinahapeni. Kama vepe tukaze wanangu ipo dei mambo yatakuwa levo.

Tudei bana ngoja niwape listori la chama langu mmoko ambaye anamaindi kitonga ile mbaya. Yaani jamaa ukitaka muende sawa basi kuwe na mteremko. Ni denja ileile kwa mtoto wa kiume kumaindisha mambo ya mtelezo kama amekanyaga ganda la ndizi iliyokwiva. Si unajua zileee…ukilikanyaga masti uteleze na kama huna stamina ndo hivo unaweza kwenda dauni kama embe dodo vile.

Sasa bana jamaa anachili kwa shem lake…yaani msela kamweka insaidi sista’ake. Mwanangu naye kajitoa kitu cha ufahamu kaenda kujiegesha kwa sista. Si umbulula huo? Yaani chama langu kwa deizi tulizonazo si mzuka hata nukta kuchili kwa shem lako hata kama laifu limekataa kiasi gani. Ikitokea iwe ishu ya mpito kinoma na siyo kumtegemea msela kwa kila kitu. Kwani unanyaka yeye katafuta vipi hadi hapo alipo? Huo ndo tunaita usnichi uliopitiliza arifu.
Mwana unaambiwa alikuwa fulu kero kwa kitaa cha bee Bongo tambarare. Selaa alikuwa akichukua ndinga la shem basi unaambiwa ni mwendo wa kupiga bakora mwanzo mwisho.

Siku ya siku si ndo shem mtu akaona isiwe kitu beta amtimbie kwenye viota vyake akiwa na kampani kwa fasi ya bata za kuungaunga. Ebana unaambiwa jamaa alimpa makavu kinoma kumbe hata zile pamba nyepesi alizotupia zilikuwa za shemeji yake!
Dah! Mazee ilikuwa ni kwere kinoma maana msela alikuwa kazungukwa na wana na mashori so ishu ya kutumbuliwa na shem lake ikawa bonge moko la nishai.

Basi bana, baada ya shemeji mtu kutambaa na ndinga huku akimwacha msela hana madaireksheni na kumpiga biti asitimbe skani kwake sasa ndo mwana akabaki kwenye krosi rodi. Aisee msela sasa hivi anaishi laifu la kuunga kinoma na wale mashori waliokuwa wanamuona mjanja wao, wanamchora tu kozi hana ishu so wameamua kama vepe wamfungie tuu kitu cha vioo.

Mmenisoma wanangu wenyewe? Acha kumaindisha ganda la ndizi mazee, ongeza spidi ya kuhaso ili kama ni kitu cha bakora, basi upige kwa kujinafasi!

Kama vepe najikataa kimtindo. Sii yuu maneksti wiki majembe yangu ya ukwehe.

Leave A Reply