The House of Favourite Newspapers

Pam D achomolea dili la kuuza unga

0

PAM DMsanii wa muziki Bongo, Pamella Daff a ‘Pam D’.

NA MAYASA MARIWATA

MSANII wa muziki Bongo, Pamella Daff a ‘Pam D’amefunguka kuwa hivi karibuni kuna jamaa alimfuata na kutaka amuingize kwenye dili la kuuza unga lakini akamchomolea.

kipiga stori na Ijumaa, Pam D alisema: “Yule jamaa alinifuata akaniambia eti kwa kuwa nakutana na mastaa wengi, anipe mchongo huo. Kwanza nilimshangaa sana, nikajiuliza kwa nini anifuate mimi.

“Kwa kuwa ni biashara ambayo sitaki hata kuisikia, nilimjia juu sana, nilifanya hivyo kwa kuwa nilijua anataka kuniingiza kwenye matatizo, mimi na unga wapi na wapi bwana.”

Leave A Reply