The House of Favourite Newspapers

PICHA : Rais JPM amkaribisha Lowassa Ikulu, Chamwino

0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mwenyekiti wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli amemualika waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowasa pamoja na mkewe Mama Regina Lowassa kwa ajili ya kupata chakula cha mchana nyumbani kwake, Ikulu ya Chamwino Dodoma. Rais Magufuli amemualika Lowassa mara baada ya mkutano mkuu wa chama cha mapinduzi uliofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa wakati alipomkaribisha nyumbani kwake Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma jana mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa jana wakati alipomkaribisha nyumbani kwake Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli kushoto katika picha ya kumbukumbu na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliyeambatana na Mkewe Mama Regina Lowassa nyumbani kwa Mhe.Rais Dkt. Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliyeambatana na Mkewe Mama Regina Lowassa nyumbani kwa Mhe.Rais Dkt. Magufuli jana mara baada ya hafla ya Chakula cha mchana aliyowaandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM.

PICHA NA IKULU

Leave A Reply