The House of Favourite Newspapers

Pluijm Ataka Kushinda Mechi Zote

Hans van Der Pluijm

KOCHA mkuu wa timu ya Azam FC, Hans van Der Pluijm, amesema kuwa mipango yake kwa sasa ni kuhakikisha kwamba wanafanikiwa kushinda mechi zote za ligi kuu ili kuweza kuibuka na ubingwa.

 

Azam wamefanikiwa kushinda mchezo wa pili katika uwanja wa nyumbani Chamazi ambao mchezo wa kwanza walicheza dhidi ya Mbeya City na kushinda kwa mabao 2-0 na mchezo wa pili ni dhidi ya Ndanda walishin­da mabao 3-0.

 

Akizungumza na Cham­pioni Jumatano, Pluijm alisema kuwa anashangazwa na uwezo wa wachezaji wake wakiwa uwanjani jambo ambalo ana imani kwamba litakuwa na matokeo mazuri katika michezo yao ya ligi kuu.

 

“Malengo yetu ni kuhak­ikisha kwamba tunafanikiwa kushinda mechi zote ambazo tutacheza nyumbani na ugenini ili kujiweka katika mazin­gira mazuri ya kuweza kuibuka na ushindi kwa kuwa hakuna mwalimu ambaye anafikiria kufun­gwa.

 

“Nidhamu kwa wache­zaji na ushirikiano ni kitu muhimu ambacho kinatupa nafasi ya kushinda kwa kuwa ushindani kwa sasa ni mkubwa baada ya timu kuongezeka ila hilo halitupi tabu kwa kuwa huwa ninaongea na wachezaji namna itakayo­saidia kuweza kupata matokeo mazuri,” alisema Pluijm.

 

Azam wame­fanikiwa kushinda michezo yao yote miwili dhidi ya Ndanda na Mbeya City ambayo yote im­epigwa Dimba la Chamazi.

Stori na Lunyamadzo Mlyuka

YANGA Wakutana Kuomba DUA Kabla ya Ligi Kuu

Comments are closed.