Pretty Kind: Nimesutwa sana kwa umbeya!
MSANII wa filamu za Kibongo, Suzan Michael ‘Pretty Kind’ amefichua siri yake kwamba alipokuwa mdogo alikuwa mbeya kiasi cha kuwafanya watu kumuogopa pale walipokuwa wakiongea mambo yao.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Prett Kind alisema kuwa alikuwa akipenda kudakia mambo ya watu wakiwa wanaongea na kuyaanika, kitu ambacho kiliwakera sana.
“Yaani umenikumbusha mbali kweli, baba yangu alikuwa hanipendi kwa sababu ya mashosti, nilikuwa na marafiki wengi nawajaza nyumbani lakini ndugu zangu walikuwa hawanipendi kwa umbeya, yaani nimesutwa sana kwa tabia hii ya umbeya,” alisema Pretty Kind.
Stor: Hamida Hassan
Comments are closed.