The House of Favourite Newspapers

Promota Semunyu: Selemani Kidunda Dhidi ya Tshimanga Katompa Rasmi Julai 30 Songea

0
Kocha wa Gym ya Naccoz , Rama Jah na wadau wengine wakiwa kwenye foleni ya kuchukua futari jana kwenye tukio la Futari ya mabondia na wadau iliofanyika jana katika Ukumbi wa 361, Mwenge.

 

PROMOTA wa mapambano kutoka Kampuni ya Peak Time Media (PTM), Meja Seleman Semunyu ameweka wazi rasmi kuwa pambano la kisasi kati ya Mtanzania, Selemani Kidunda dhidi ya Mkongomani Tshimanga Katompa linatarajiwa kupigwa Julai 30, mwaka huu Songea mkoani Rukwa.

Bondia Mfaume Mfaume akiwa kwenye foleni ya kuchukua futari jana.

Pambano hilo litakuwa la pili kwa mabondia hao kukutana ambapo mwezi Desemba mwaka jana walipambana jijini Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya TKO, kufuatia Kidunda kupata jeraha la kupasuka usoni.

 

Semunyu aliyasema hayo katika iftar maalum iliyoandaliwa na Peak time Media kwa wadau mbalimbali wa mchezo wa ngumi, iliyofanyika juzi Alhamisi jijini Dar es Salaam.

 

Meja Semunyu alisema: “Baada ya kuwepo kwa mahitaji ya wadau wengi wa ngumi juu ya kutaka kujua nani mbabe kati ya Kidunda na Katompa sisi tumewasikia na sasa tunawatangazia rasmi kuwa pambano hilo la kisasi litapigwa Julai 30, mwaka huu, Songea mkoani Rukwa hivyo tunaomba sapoti yenu.”

Baadhi ya akina mama na mabondia wakike ambao wamejitokeza kwenye Futari.
Baadhi ya mabondia na makocha wakiwa katika picha  ya pamoja na viongozi wa Kampuni ya Peak Time Media mara baada kupata futari jana kwenye Ukumbi wa 361, Mwenge.

Baadhi ya wadau wakiwa kwenye sala ya Magharibi kabla kupata futari jana jioni.

Leave A Reply