The House of Favourite Newspapers

Rais Magufuli amsimamisha kazi kamishna wa TRA

451Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Rished Bade.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania, Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli amemsimamisha kazi kuanzia jana tarehe 27 Nov. 2015, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Rished Bade kufuatia ziara ya kushtukiza ya Waziri Mkuu, Mh. Majaliwa Kasimu Majaliwa mapema jana asubuhi Bandarini jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akizungumza na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari (hawapo pichani) kuhusu upotevu wa makontena zaidi ya 349 huku akiwa ameshika nyaraka yenye orodha ya makontena hayo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akionesha nyaraka hiyo mbele ya waandishi wa habari waliofika kwenye mkutano huo.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue wakwanza kushoto akifafanua jambo mbele ya wanahabari.

Comments are closed.