Rais Magufuli apiga simu ‘live’ Clouds 360
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kewe Mama Janeth Magufuli leo asubuhi wamepiga simu moja kwa moja katika kipindi cha Clouds 360 na kuwapongeza watangazaji wa kipindi hicho kwa kazi nzuri wanayoifanya.
Rais Magufuli alisema kuwa yeye ni shabiki namba moja wa kipindi hicho na anafurahishwa na kazi nzuri inayofanywa na Clouds Media Group kama zoezi zima la ‘Malkia Wa Nguvu’ na mengine mengi. Wakiongea na watangazaji wa Clouds 360, waliwataka nao wakati mwingine waje na wenzi wao katika kipindi na si kila mara waje wenyewe .
Wafanyakazi hicho walimshukuru rais kwa kitendo chake hicho chenye kuonyesha kuwa wanaifanya kazi yao vizuri lakini pia wanasema ilikuwa faraja kwao kwani wanaamini kituo hicho kimekuwa cha kwanza kwa rais kufanya kitendo hicho.
Mmedhihirisha ni wazalendo mpaka raisi magufuli kawapa tano hongera sana