RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA QURAAN (PICHA +VIDEO)
PICHA NA IKULU
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametoa zawadi mbalimbali za washindi wa mashindano ya 20 ya kusoma na kuhifadhi Quran Afrika yaliyofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar, leo.
Katika hotuba yake, Magufuli amesema anafahamu uwepo wa watu wenye tamaa ya kupandisha bei katika kipindi cha Mfungo wa Ramadhani hivyo amewataka kuacha tabia hiyo mara moja.
Amesema kufanya hivyo ni dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu kufanya hivyo hakuwezi kumtajirisha mtu hasa kwa kupandisha bei ya vile vitu vinavyotumika sana katika mfungo huu.
“Nitumie fursa hii kutoa wito kwa mamlaka husika za Serikali kufuatilia suala hili kwa ukaribu sana,” amesema Magufuli.
Mbali na hilo amewataka watu wa madhehebu mengine na wale wasiokuwa na dini kuendelea kushirikiana na Waislam katika kutimiza mfungo wa mwezi huu ambao ni moja ya nguzo tano za Uislam.
“Namuomba Mungu awalipe malipo stahiki juu ya kile mnachokifanya katika funga zenu. Mimi mwenyewe sijafunga, lakini siku ya kufumgua Waislam nitakua nanyi katika pilau,” amesema.
Comments are closed.