Rais Samia Afanya Uteuzi wa Mkuu Mpya wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF)
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amempandisha Cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda kuwa Jenerali na amemteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (Chief of Defence Forces-CDF)
Wakati huohuo Rais Samia amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Majeshi aliyemaliza muda wake Jenerali Venance Salvatory Mabeyo alipokwenda kumuaga Ikulu jijini Dar es Salaam.