Rais Samia Aongoza Kuaga Mwili wa Mhandisi Mfugale-Picha
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameongoza waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), mhandisi Patrick Mfugale inayofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mfugale alifariki dunia Jumanne Juni 29, 2021 saa 5 asubuhi katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.
Mwili wa Mfugale unaagwa leo Ijumaa Julai 2, 2021 katika viwanja hivyo kabla ya kusafirishwa kwenda Ifunda mkoani Iringa kwa mazishi yatakayofanyika nyumbani kwake Julai 5, 2021.
Kwa mujibu wa ratiba baada ya kutoa heshima ya mwisho, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Kimara Temboni,baada ya misa takatifu siku ya Jumamosi Julai 3, 2021 atasafirishwa kwenda Ifunda mkoani Iringa kwa ajili ya maziko yatakayofanyika Julai 5, 2021.