The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Atangaza Kuwajengea Nyumba Walioathirika Na Mafuriko Manyara, Atoa Maagizo (Picha +Video)

0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waathirika wa Mafuriko waliopo kwenye kambi zao Katesh, Wilayani Hanang mkoani Manyara

 

Rais Samia Suluhu Hassan, amesema wataalam wa serikali, tayari wametenga eneo ambalo litatumika kuwahamisha waathirika wa maporomoko ya tope, Hanang mkoani manyara ambapo itawaunga mkono katika ujenzi wa makazi mapya ya kudumu.

Pia amezitaka taasisi za serikali kuwa na utaratibu wa kuchunguza kwa makini majanga ya asili kabla hayajatokea na kuchukua tahadhari ili kuepusha madhara kama yaliyotokea Hanang.

Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waathirika wa Mafuriko waliopo kwenye kambi zao Katesh, Wilayani Hanang mkoani Manyara
Rais Samia akiendelea kuzungumza na Waathirika wa Mafuriko waliopo kwenye kambi zao Katesh, Wilayani Hanang mkoani Manyara
Rais Samia akiwa amembeba mtoto Wina Joseph mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 8 ambaye pia yeye na mama yake ni waathirika wa mafuriko yaliyotokea Katesh Wilayani Hanang. Rais Samia aliwatembelea majeruhi wa maafa ya mafuriko hayo ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tumaini, Hanang Mkoani Manyara tarehe 7 Desemba, 2023.
Rais Samia akiwa ndani ya Helikopta na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga wakati wakiangalia athari za mafuriko yaliyotokea katika mji mdogo wa Katesh pamoja na vijiji jirani, Hanang Mkoani Manyara tarehe 7 Desemba, 2023
Rais  Samia akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga akielezea kuhusiana na athari za mafuriko yaliyotokea katika eneo la Jorodom Katesh Wilayani Hanang. Rais Samia ametembelea eneo hilo Mkoani Manyara tarehe 7 Desemba, 2023.


Leave A Reply