Rais Samia Atembelea Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma nchini Indonesia
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Januari Makamba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo pamoja na viongozi wengine leo Januari 26, 2024 wametembelea Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma nchini Indonesia wakati akihitimisha ziara yake nchini humo.