Rais Samia Awasili Namibia kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Rais wa Namibia Marehemu Dkt. Hage Geingob
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili nchini Namibia kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Rais wa Namibia Marehemu Dkt. Hage Geingob, tarehe 23 Februari, 2024. Shughuli za Mazishi za Rais huyo Hayati Dkt. Hage Geingob zitafanyika katika Jiji la Windhoek tarehe 24-25 Februari, 2024.