The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Azindua Minara ya Urushaji wa Matangazo ya Televisheni kwa Kutumia Antena

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na Wafanyakazi wa Azam Media mara baada ya kufungua Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Kampuni hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika Ofisi za Kampuni hiyo zilizopo Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2023.
Rais Samia akimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited Ndugu Tido Mhando wakati alipotembelea Studio za matangazo za Azam TV zilizopo Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam.
Rais Samia akibonyeza Kitufe kuashiria ufunguzi wa Mradi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) .
Rais Samia akifurahia jambo na Mtoto Georgina Magesa (8) mara baada ya kuonana na  Rais.
Rais Samia akifurahia jambo wakati Mtoto Georgina Magesa (8) akiwa ameketi kwenye Kiti cha Rais mara baada ya kukutana naye katika hafla ya uzinduzi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Azam Media iliyofanyika katika Ofisi zao zilizopo katika Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam
Rais Samia akipokea zawadi ya King’amuzi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Ndugu Abubakar Said Salim Bakhresa kwa ajili ya kuangalia maudhui mbalimbali ya Azam TV mara baada ya kuzindua mradi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Kampuni hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika Ofisi zao zilizopo Barabara ya Mandela Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2023
Rais Samia akimkabidhi Tuzo kwa Niaba ya Kampuni ya Azam Media Mama Violet Maro Mwanamke wa kwanza Mwandamizi katika fani ya Habari nchini wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa Minara ya kurusha matangazo ya Televisheni Ardhini (DTT) ya Kampuni ya Azam Media Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2023

Rais Samia Suluhu Hassan leo Mei 18, 2023 amezindua minara ya mfumo wa urushaji wa matangazo ya televisheni kwa kutumia antena, yaani mfumo wa Digital Terrestrial Television (DTT).

Minara hiyo iliyojengwa kwenye mikoa 21 na kugharimu jumla ya shilingi bilioni 50 imejengwa katika kipindi cha miaka miwili na miezi sita.

Kwa kuwa na idadi hiyo kubwa ya minara, Azam Media Limited inaongoza kuwa kampuni ya kwanza nchini kwa minara ya Televisheni.

Rais Samia amefanya uzinduzi huo kwenye studio za Azam TV Dar es salaam.

Ahmed Abdalah ambae ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Teknolojia na Miundombinu ndiye mratibu wa mradi huu mkubwa.

Leave A Reply