The House of Favourite Newspapers

Rais Wa Etihad Ahutubia Kongamano la Huduma za Mizigo, Abu Dhabi‏

0

James Hogan - PCEO Etihad AirwaysRais na afisa mkuu wa shirika la ndege la Etihad, bwana James Hogan alitoa hotuba ya ufunguzi mbele ya zaidi ya wajumbe 1,200 waliohudhuria kongamano kuu la masuala ya huduma ya mizigo lilofanyika katika kituo cha maoneyesho cha Abu Dhabi kuanzia tarehe 10 hadi 13 Machi.

Bwana Hogan aliongelea kiundani juu ya mabadiliko katika sekta ya mizigo na jinsi gani muungano wa washirika wa shirika la ndege la Etihad umeongeza nguvu katika utendaji kazi wa kitengo hicho cha mizigo. Kwa kuunganisha ndege za mizigo na mitandao yake, kitengo cha mizigo cha Etihad kinatambulika kama kitengo namba tano (5) kwa ukubwa duniani kikishirikiana kwa ukaribu wa dhati na kitengo cha mizigo cha shirika la ndege la Jet, kitengo cha mizigo cha shirirka la ndege la berlin, Serbia, Alitalia, na kitengo cha mizigo cha shirika la ndege la Seychelles.

Kitengo cha mizigo cha shirika la ndege la Etihad hutengeneza zaidi ya dola bilioni 1 za kimarekani kama mapato ya mwaka na kukifanya kuwa  moja ya kitengo cha mizigo chenye mafanikio zaidi duniani.  Kilifanikiwa kuhudumia asilimia 88 ya mizigo yote iliyoingia, iliyotoka na iliyosafirishwa  katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abu Dhabi mwaka 2015, mwaka ambao kitengo hicho kilibeba tani 529,090 za mizigo na barua, jumla ikiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 4 ya mwaka 2014.

Kwa sasa kitengo cha mizigo cha Etihad kwa kutumia ndege nne aina ya boeing 777F, tatu aina ya boeing 747s, na nne aina ya airbus A330s. ndege iliyoongezwa aina ya  boeing 777 inatazamiwa kuwasili ndani ya mwezi huu uku nyingine aina ya airbus A330 ikiwa imepangwa kuwasili mwaka 2017.

Bwana Hogan alizungumzia jinsi gani Kanda ya Mashariki inaendelea kufanya vizuri katika viwango vya ukuaji wa kimataifa kwenye sekta ya mizigo na ina jukumu muhimu katika mtiririko wa biashara na bidhaa duniani, pamoja na umuhimu wake wa kijiografia kuimarika kutokana na wadau kuhama masoko ya zamani yaliojazana na kuanzisha masoko mapya katika vituo vya biashara huko Mashariki ya Kati, Asia, Amerika ya Kusini na Afrika.

Alisema: “Kitovu chetu cha Abu Dhabi ni njia panda ya dunia chenye kitengo kikubwa cha kushugulikia mizigo, Shirika la ndege la Etihad  limejiweka nafasi nzuri kunufaika na ongezeko la abiria, ongezeko la mizigo na bidhaa zinazosafirishwa baina ya masoko makubwa na yale mapya”

Etihad Cargo inatoa huduma ya kubeba mizigo kawaida ndani ya ndege pamoja na kwenye buti la ndege huduma hizi zikifikia mtandao wa abiria pamoja na vituo vya mizigo tu.

“Kitengo cha mizigo cha Etihad kimekuwa biashara inayoingiza mapato ya mabilioni na inawakilisha sehemu kubwa ya biashara yetu kwa kujidhatiti kutoa huduma maalumu kwa wateja pamoja na bidhaa zenye ubunifu zenye kutoa ushindani mkubwa na kuvutia wateja wetu. Kwa kufanya kazi na washirika wetu, tutaendelea kuongeza faida ya kila kituo cha mizigo kwa kuchanganya rasilimali, mitandao na uwezo kwa manufaa ya wateja wetu wote “alisema Bw Hogan.

Ushirikiano na watendaji wengine wa mizigo, zikiwemo Atlas Air na Avianca, hutoa msaada mkubwa kwa kituo kikuu, na kitengo kinaendelea fursa za ushirikiano na vitengo vingine vya waendeshaji mizigo. Shirika kwa hivi sasa linafanya kazi katika vituo 14 vinavyojihusisha na mizigo tu ikiwa ni pamoja na Bogotá, Brazzaville, Chittagong, Djibouti, Dubai World Kati, Eldoret, Guangzhou, Hanoi, Houston, Sharjah na Tbilisi.

Leave A Reply