The House of Favourite Newspapers

Rais Wa Zanzibar Dk Shein Atangaza Kuongeza Mishahara – Video

0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar

Hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwenye maadhimisho ya miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar zimefanyika leo Jumapili Januari 12, 2020 katika Uwanja wa Abeid Aman Karume.

 

Rais Shein amesema kutokana na makusanyo mazuri ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar anaweza kuongeza mshahara kwa Watumishi kama jinsi marekebisho ya maslahi ya Wafanyakazi ya mishahara yalivyofanywa mwaka 2011, 2013,2015 na 2017.

Baadhi ya aliyoyasema kwenye hotuba yake:-

“Kila tunapoikumbuka siku hii muhimu tunapaswa tuwakumbuke viongozi wetu waliopigania taifa, wakiongozwa na jemedari wetu mzee Amani Abeid Karume. Tunamuomba Mungu awalaze mahali pema peponi waasisi wetu wa Mapinduzi”

“Serikali ya awamu ya saba ndani ya miaka 9 imeendelea kutekeleza mipango ya mageuzi ya kiuchumi kwa kuimarisha hali ya amani na kuongeza pato la uchumi mara sita zidi. Kutoka Trilioni 1.78 mwaka 2010 Trilioni 2.87 mwaka 2018”

“Kutokana na hali nzuri tunayokusanya, msishangae na mwaka huu nikikuongezeeni chochote kwa lengo la kuwapa motisha Wafanyakazi”.

Mgeni rasmi,Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais Mstaafu wa Zanzibar wa awamu ya sita Dk. Amani Abeid Karume alipowasili jukwaa kuu,katika Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar.Pichani kati anaeshuhudia ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.
VIJANA wa Maandamano Maalum ya kuadhimisha Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwa na Picha za Waasisi wa Mapinduzi, wakati wa hafla hiy0 iliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Vijana wa Chama cha mapinduzi wakipita mbele ya Mgeni Rasmi ikiwa ni Ishara ya kutoa heshima katika maandamano ya maadhimisho ya ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman mjini Zanzibar
Wanachama wa Chama cha CUF wakishiriki katika Maandamano ya kuadhimisha sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi Zanzibar zilizofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar
Vijana wa payunia wakitowa salamu ya heshima kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein wakati wa maandamano ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akitoa hotuba ya kilele cha Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman mjini Zanzibar.

 

Leave A Reply