Rayvanny Amposti Mpenzi Wake Paula
Kwa mara ya kwanza, staa wa Bongo Fleva, Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’ amemposti mpenzi wake Paula akiwa anaonekana sura vizuri.
Miezi kadhaa iliyopita, Rayvanny alimposti mrembo huyo akiwa amewapa mgongo wambeya na picha hiyo akawa ameiweka ‘black&white’ ili kuwafanya wambeya wasiweze kung’amua haraka.
Usiku wa kuamkia leo, Rayvanny ameamua kumposti kwa kumuonesha sura na picha ya rangi saafi kabisa na hakuandika maelezo yoyote. Hii inaitwa ‘penzi ni kikohozi, kulificha huwezi.’
Stori: Erick Evarist