RC wa Iringa Ally Hapi akizunguzmia sakata la Chama cha Wanahabari wa Mkoa wa Iringa kumpa siku 7 aombe radhi baada ya kuwataka nao kuwa na vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo.
Jumatatu ya Mei 27 wakati akiuzungumza na watendaji, Hapi alisema… “Wafanyabiashara ni wengi kuna wapiga debe, wauza nyanya, mchicha, wachoma mahindi na hata waandishi wa habari na wapiga picha wote wanatakiwa kuwa na vitambulisho ili kuchangia kodi kutokana na kazi wanazofanya.”
Akizungumzia kutakiwa kuomba radhi, Hapi amesema yeye kama Mkuu wa Mkoa anamwakilisha Rais Magufuli, hivyo hakuna mtu wa kumpa siku saba Rais kwa mumwamuru afamye jambo flani.
Comments are closed.