Mbunge wa Jimbo la Chalinze,Mhe. Ridhiwan Kikwete jana Agosti 6, 2021 ameendelea na ziara yake katika Tarafa ya Miono kwa kufanya mikutano na Wananchi kuzungumzia maendeleo ya maeneo yao na namna bora ya kuyaendeleza ambapo pia alipata fursa ya kuwashauri wananchi namna kuchukua tahadhari zinazotolewa na Wizara ya Afya ya kujikinga na Ugonjwa wa Corona ikiwemo kupata Chanjo ili kujikinga na Covid 19. #KaziIendelee #ChalinzeIendelee