Ronaldo Ajinafasi Ugiriki ‘Akisubiri’ Kujiunga Juventus
WAKATI kuna uvumi mkubwa wa nyota wa soka wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, kujiunga na Juventus ya Italia, Mreno huyo hivi sasa, tangu jana Jumatatu, yuko Ugiriki akila bata na mshikaji wake aliyejulikana kwa jina la Georgina Rodriguez.
Mashuhuda wanasema Ronaldo ana kundi la watu wapatao 15 hadi 20 ambao ni pamoja na ndugu na watoto wa familia yake.
Juventus inategemewa kumnunua nyota huyo kwa Dola mil. 450 ambazo ni sawa na Sh. bil. 1.5, kumtoa katika klabu hiyo aliyoitumikia kwa misimu tisa, ambapo atawatumikia waajiri wake hao wapya hadi mwaka 2022.
Comments are closed.