The House of Favourite Newspapers

Ronaldo Anyakuwa Ballon d’Or, Awavurugua Messi, Griezmann na Suarez

 ronaldo-ballon-dor-2  
BILA ubishi, unaweza kusema huu ni mwaka wa Cristiano Ronaldo hata kama unakwenda ukingoni. Hii inatokana na mafanikio makubwa ambayo ameyapata kwa mwaka huu wa 2016 ambapo kubwa zaidi ikiwa ni kushinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia maarufu kama Ballon d’Or ambayo ilifanyika Paris, Ufaransa, usiku wa jana Jumatatu Desemba 12, 2016.

ronaldo-ballon-dor-1Ronaldo sasa anaichukua mara ya nne, akiwa alianza mwaka 2008 akiwa Manchester United na alipoingia Madrid, unaweza kusema hii ni ‘hat trick’.

Kabla haijawa Ballon d’Or, Ronaldo alichukua mwaka 2008, Messi akachukua mwaka 2009.

Baada ya kuwa Ballon d’Or, Messi amechukua mara nne miaka ya 2011, 2012, 2013 na 2015. Huku Ronaldo akiwa amechukua mara tatu katika miaka ya 2013, 2014 na 2016.

ronaldo-ballon-dor-2Kumbuka alishinda Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Klabu yake ya Real Madrid, akashinda Kombe la Euro akiwa na Timu yake ya Taifa ya Ureno.
Jana  amebeba kura zaidi kati ya 173 zilizopigwa na waandishi duniani kote kwa usimamiza wa jarida maarufu la Ufaransa la France Football na kuwapiga bao Antoine Griezmann wa Atletico Madrid na Luis Suarez na Lionel Messi, wote wa Barcelona.

ronaldo-ballon-dor-32016 BALLON D’OR RESULT

1. Cristiano Ronaldo (Portugal / Real Madrid)

2. Lionel Messi (Argentina / Barcelona)

3. Antoine Griezmann (France / Atletico Madrid)

4. Luis Suarez (Uruguay / Barcelona)

5. Neymar (Brazil / Barcelona)

6. Gareth Bale (Wales / Real Madrid)

7. Riyad Mahrez (Algeria / Leicester City)

8. Jamie Vardy (England / Leicester City)

9. Pepe (Portugal / Real Madrid)

9. Gianluigi Buffon (Italy / Juventus)

11. Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon / Borussia Dortmund)

12. Rui Patricio (Portugal / Sporting Lisbon)

13. Zlatan Ibrahimovic (Sweden / Manchester United)

14. Arturo Vidal (Chile / Bayern Munich)

14. Paul Pogba (France / Manchester United)

16. Robert Lewandowski (Poland / Bayern Munich)

17. Dimitri Payet (France / West Ham)

17. Luka Modric (Croatia / Real Madrid)

17. Toni Kroos (Germany / Real Madrid

France Football’s imeanika kati ya wachezaji 30, hawa 11 hawakupata kura hata moja: Aguero, De Bruyne, Dybala, Godin, Higuain, Iniesta, Koke, Lloris, Muller, Neuer na Ramos.

ronaldo-ballon-dor-3LAST 10 WINNERS

2007 – Kaka

2008 – Cristiano Ronaldo

2009 – Lionel Messi

2010 – Lionel Messi

2011 – Lionel Messi

2012 – Lionel Messi

2013 – Cristiano Ronaldo

2014 – Cristiano Ronaldo

2015 – Lionel Messi

2016 – Cristiano Ronaldo

ronaldo-ballon-dor-1RONALDO’S 2016

Kimataifa:

Mechi – 13

Magoli- 13

Assists – 3

Klabu:

Mechi – 42

Magoli- 38

Assists – 14  

Mataji – Champions League, UEFA Super Cup, Euro 2016

rap

halotel-strip-1-1

Comments are closed.