Safu ya Ulinzi Tatizo Mbeya Kwanza
KOCHA Msaidizi wa Mbeya Kwanza, Nizar Khalfan, amefunguka kuwa umakini mdogo kwenye safu yao ya ulinzi
imekuwa sababu kubwa kwa kikosi chake kupata matokeo yasiyoridhisha kwenye Ligi Kuu Bara.
Mbeya Kwanza imeruhusu mabao 16 katika michezo 14 waliyoshuka dimbani hadi sasa ikishika nafasi ya tatu kwa timu zilizoruhusu idadi kubwa ya mabao kwenye ligi msimu
huu.
Akizungumza na Spoti Xtra, kocha huyo alifunguka kwamba: “Tumeichukua timu ikiwa kwenye kipindi kigumu,
kuna changamoto nyingi katika maeneo mengi kikosini, tumeruhusu mabao mengi mepesi ambayo yametokana na udhaifu kwenye eneo la ulinzi.
“Tunaendelea kulifanyia kazi ili tuweze kuwa na timu imara kwani hatupo katika nafasi nzuri kwenye msimamo, hivyo tunahitaji kupambana kujiondoa huko na njia pekee ni kupata matokeo mazuri kwenyemechi zote zilizosalia.”
Kabla ya mechi za jana, Mbeya Kwanza ilikuwainashika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi
Kuu Bara ikiwa na pointi 13, imeshinda mechi mbili, sare saba na kupoteza tano.
STORI NA HUSSEIN MSOLEKA | SPOTI XTRA