The House of Favourite Newspapers

Saido: Nitawapa Ubingwa Yanga SC

0

WAKATI jana Jumamosi akitarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu Bara akiwa na Yanga, kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mrundi, Saido Ntibazonkiza ‘Saido’ amefunguka kuwa anaona kabisa msimu huu atakuwa sehemu ya kikosi hicho kitakachotwaa ubingwa.

 

Saido alisema amegundua kuwa Yanga ni moja kati ya timu bora yenye wachezaji wenye uchu wa kutaka mafanikio ndiyo maana kila mchezo wanaocheza huwa wanajitoa kwa asilimia 100 na kupambana hadi mwisho kuhahakisha ushindi unapatikana.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Saido alisema: “Wakati nakuja hapa sikuwa nafahamu kiundani nitakutana na watu wa aina gani, kiukweli nimehamasika sana baada ya kukuta kila mtu ndani ya Yanga analia na ubingwa, hiyo imepelekea kwenye kila mchezo wachezaji kujitolea hadi mwisho.

 

Hali hiyo imenifanya hata mimi sasa kutamani kuipa ubingwa timu hii na Mungu akipenda msimu huu tutakuwa mabingwa.”

STORI: ISSA LIPONDADar es Salaam

Leave A Reply