Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa mkutano wa Kampeni uliofanyika Tabata shule Jijini Dar es Salaam,amesema kuwa.
“Ndugu zangu tunatambua changamoto za miundombinu kwenye Jiji hili, na ndio maana tunajenga Barabara za juu, madaraja na mifereji, Daraja la Salenda linaendelea vizuri, interchange ya ubungo tunakaribia kumaliza na tumetenga fedha zaidi ya bilioni 32 za mifereji ili kuzuia mafuriko”alisema Samia.
“Tumejenga machinjio ya kisasa ya vingunguti ambayo huiingizia Serikali pato la zaidi ya sh. Milioni 100 kwa mwezi, alisema tayari zimetengwa shilingi Bilioni 12.49 ambapo hadi kufikia Septemba 30, mashine za kisasa za uchinjaji zitakuwa zimefungwa.
Kwenye suala la elimu Mh.Samia alisema kuwa wametenga takribani shilingi Bilioni 44.5 kuboresha sekta hiyo kwa kujenga madarasa, ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia.
Amesema pia uboreshaji wa miundombinu katika sekta ya utalii Jiji hilo litajenga ukumbi mkubwa wa kisasa wa kitalii ambao utajumuisha hoteli, huku mikakati ya kutengeneza gati kwa ajili meli kubwa za kitalii ikifanywa.
Aidha pia alisema Serikali inaendelea kuboresha ukusanyaji wa mapato yatokanayo na utalii.