The House of Favourite Newspapers

Serikali Yatenga Bil 7 Kukabili Saratani ya Kizazi, Matiti

 

samia-hassan

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu akiongea na wakazi wa Mwanza.

rais-wa-mewata-sarafina-mkuwa

Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA), Sarafina Mkuwa akiwataka akina mama na mabinti  mkoani Mwanza kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi.

makamu-wa-rais-samia-hassan-akiteta-jambo-na-wazir-wa-afya-ummy-mwalimu-wakati-wa-uzinduzi-wa-upimaji-wa-saratani-ya-mlango-wa-kizazi-na-matiti-mwanza

Makamu wa Rais, Samia Hassan akiteta jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa upimaji wa saratani ya mlango wa kizazi na matiti Mwanza.

wananchi-waliojitokeza-kupima-saratani-katika-uwanja-wa-furahisha-mwanza

wananchi-wa-mwanza

Wananchi waliojitokeza kupima saratani katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.

baadhi-ya-manesi-wakiwa-kwenye-viwanja-vya-furahisha-mwanza

Baadhi ya manesi wakiwa kwenye Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.angelina-mabula

Angelina Mabula akiongea na wakazi wa Mwanza.

JUMLA  ya Sh. Bilioni 7 zimetengwa na serikali ili kukabiliana na magonjwa ya saratani ambayo yamekuwa yakichangia kwa kiasi kukubwa vifo vya kina mama na mabinti. Hii ni kutokana na  watu hao kupoteza maisha kwa ugonjwa huo  kwa  kukosa fedha za  matibabu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa   kampeni  ya kuhamasisha upimaji wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi kwa akina mama na mabinti jijini hapa jana, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu,  alieleza kuwa  mwaka jana serikali ilikuwa imetenga Sh. Billion moja na kwamba kwa  sasa kiwango hicho kimeongezwa  ili kukabilina na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo sugu.

“Tumejitahidi  kwa kiasi kikubwa  katika  serikali hii ya awamu ya tano kuhakikisha tunaboresha afya ya mama na mtoto lakini pia kuhakikisha tunasaidia kutibu magonjwa hayo sugu ambayo yanaendelea kuwa tishio kwa wanawake hasa kwenye nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania”,  alisema Samia.

Aidha aliwapongeza madaktari wote nchini katika kujitoa na kuhakikisha wanaokoa maisha ya Watanzania katika sekta zote kama macho, migongo-wazi, moyo na kuwataka kuendelea na moyo huohuo licha ya kufanya kazi kwenye mazingira magumu.

Aliongeza kuwa serikali imetoa kipaumbele kwa magonjwa hayo kutokana  na idadi ya wangojwa wa  saratani ya mlango wa kizazi kufikia  asilimia 38, huku saratani ya matiti ikiwa ni asilimia  12,  saratani ya koo ikiwa na asilimia tisa, kichwa na shingo 7, matezi 5.4, damu 4.7 na kibofu cha mkojo asilimia tatu.

Alieleza kuwa aidha serikali haijasahau magonjwa ya tezi dume kwa wanaume kutokana na kwamba ndani ya mwezi mmoja wanaume saba waliobainika kuwa na ugonjwa huo wanne wamefariki dunia.

Awali Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA), Sarafina Mkuwa, aliwataka kina mama na mabinti  mkoani hapa kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi ili watakaogundulika waaze matibabu haraka.

“Ugonjwa huu unatibika ukiwahi  kupima na kugundulika hivyoa niwatake kina mama wenzangu wapunguze unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara, kuwa na wapenzi wengi  na kuanza mapenzi katika umri mdogo kuwa ndiyo uchangiaji mkubwa wa kirusi kiitwacho Human Papromal (HPV).

Aidha alivitaja vituo vinne vitakavyokuwa vinatoa huduma kwa siku mbili jijini hapa kuwa ni Furahisha, Makongoro, Igoma na Karume lengo lake kubwa likiwa ni kupima kina mama 3,000 upande wa saratani ya matiti na 1,200 saratani ya mlango wa kizazi.

Naye Mganga mkuu wa Mkoa wa Mwanza,  Dk. Leornad Subi,  alisema kuwa mwaka jana kati ya wagonjwa 1,6000 waliofanyiwa uchunguzi  wa awali, 333 wamegundulika  kuwa  na ugonjwa huo, ambapo  185 wakipewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Rufaa Bugando na 66 wakiwahishwa kwenye Hospitali ya Ocean Road.

Na Idd Mumba, Mwanza

Comments are closed.