The House of Favourite Newspapers

Serikali Yatoa Bei Elekezi ya Sukari kuwa ni Sh. 1800 Nchi Nzima

2

sukari Mkurugenzi  mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania, Henry Semwaza

HATIMAYE  Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli  imekisikia kilio cha muda mrefu  cha Wananchi ambao  walikuwa wakilalamika kupanda  kwa  bei ya sukari nchini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari  mchana huu  jijini Dar es Salaam Mkurugenzi  Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania, Henry Semwaza amesema kuanzia sasa kilo moja ya  sukari itauzwa kwa sh.  1800 nchi nzima.

“Serikali, kupitia bodi ya Sukari Tanzania, inawaarifu wananchi wote kuwa bei ya rejareja ya sukari sasa itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja
. “Amesema Semwaza na kuongeza;

” Wafanyabiashara wote wanapaswa kuzingatia agizo hili, pamoja na kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi bila kuihodhi.

“Maafisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia na kusimamia utekelezaji wa agizo kuhusu bei elekezi ya sukari, na hawatasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale watakaobainika kupandisha bei ya bidhaa hiyo. “

AGIZO LA SERIKALI KUHUSU BEI ELEKEZI YA SUKARIsukari

2 Comments
  1. Nsolo S. Stephen says

    Huu ni ukombozi kwa wananchi!

  2. Nsolo S. Stephen says

    Taarifa hii inaagiza kilo 1 = Tsh. 1800/= NCHI NZIMA kwa maana ya popote Tanzania!
    Sijui kama itatekelezeka huko ndani ndani vijijini.

Leave A Reply