The House of Favourite Newspapers

Shamsa Amkingia Kifua Uwoya

MREMBO wa Bongo Muvi, Shamsa Ford amemkingia kifua muigizaji mwenzake Irene Uwoya baada ya watu kumtolea maneno machafu kwenye mtandao wa kijamii kuhusiana na vazi alilovaa la ufukweni.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Shamsa alisema kuwa watu wa kwenye mitandao ya kijamii siku zote hawana jema unaweza kufanya kitu kizuri lakini mwisho ya yote likaonekana sio jambo jema hivyo vazi alilovaa Uwoya kwake haoni kama lina shida yoyote.

“Watu wanamtukana Uwoya, kwa vile tu nafikiri hawaelewi sidhani kama Uwoya kuna kosa alilofanya kuvaa nguo ile labda angepita nalo barabarani ingekuwa ni tatizo lakini yopo ufukweni kuna shida gani?” alihoji Shamsa.

Uwoya alizua gumzo kwenye mitandao ya kijamii wiki iliyopita baada ya kutupia picha mbalimbali zilizomuonesha akiwa kwenye vazi linaonesha maungo yake ya ndani kwa urahisi.

IMELDA MTEMA

Comments are closed.