The House of Favourite Newspapers

SHAMSA FORD ALIA NA VIBENTEN

0
Shamsa katika pozi matata

NYOTA wa filamu nchini, Shamsa Ford, ametoa ushauri kwa vijana wa kiume wa Kitanzania wenye tabia ya ‘ganda la ndizi kuteleza’, yaani wasiopenda kufanya kazi, badala yake wanatumia miili yao kama kitegauchumi kwa kujihusisha kimapenzi na mijimama yenye pesa ili wapate hifadhi hapa mjini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shamsa ameandika ujumbe maalum kwa ajili ya vijana wenye tabia hizo wanaojulikana zaidi kwa jina la Vibenten.

“Kaka zangu na wadogo zangu wa kiume ningependa kuwashauri mpende kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Msitamani kazi ya kuzunguka kwenye kiti ofisini wakati elimu yako ni darasa la pili. Mwanamme unatakiwa ujitume na kupambana na maisha.  Sukuma hata mkokoteni ilimradi ujipatie riziki.

“Sasa nyie kaka zangu wa sasa hivi yaani hampendi kufanya kazi. Ukishajiona una sura nzuri basi na wewe eti unadanga kwa jimama lenye pesa.  Sasa kama mwanamke anakufuga wewe unadhani atakuheshimu? Utachezea kuchapwa vibao na kutukanwa. Hivi hamuumii na haya majina mnayoitwa?  Mara vibenteni, vipanya buku, vichura, vitom na Jerry. Daaa inauma!”

NA ISRI MOHAMED/GPL

 

Leave A Reply