Shamsa: Siachiki kwa Chid Mapenzi
Stori: Imelda Mtema
MTOTO mzuri Bongo Muvi, Shamsa Ford ametikisa kinywa chake na kusema, wanaomuombea aachike kwa mpenzi wake, Chid Mapenzi, wanajisumbua kwani kamwe hataachika.
Shamsa aliyewahi kubanjuka kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego, kisha kutua kwa Chid, amesema kuna watu wanamtaribia kuwa uhusiano huo utavunjika lakini watasubiri sana.
“Licha ya watu kuniombea niachane na Chid hilo haliwezekani, watasubiri sana,” alisema Shamsa.