The House of Favourite Newspapers

Sheikh Jalala: Dunia Tuikumbuke Palestina

0

SAM_9690

Sheikh Hemed Jalala akizungumza na wanahabari wakati wa maadhimisho ya Siku ya QUDS ndani ya Msikiti wa Kigogo Post jijini Dar es Salaam.

Wakati waumini wa dini ya Kiislam  duniani na nchini Tanzania wakiendelea na mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, wito umetolewa kwa viongozi wa kidini pamoja na vyombo vya umoja wa mataifa kuhakikisha kuwa wanarudisha hali ya amani katika nchi ya Palestina ambayo wananchi wake wamekuwa wakiishi katika mateso, dhuluma na hali ngumu kutoka kwa nchi ya Israeli na kuwafanya wananchi wa hao kushindwa kufurahia kuishi katika nchi yao.

Wito huo umetolewa na Kiongozi Mkuu wa Dhehebu la Shia nchini Tanzania kutoka Msikiti wa Kigogo Post uliopo jijini Dar es Salaam, Sheikh Hemed Jalala wakati wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya QUADS duniani ambayo ni siku inayotumika kuwakumbuka na kutafakari kwa pamoja mateso na mambo mbaya wanayopitia wananchi wa Palestina.

SAM_9715

 Baadhi ya waumini wa dini ya Kislam wakipata semina juu ya siku hiyo ya QUDS katika Msikiti wa Kigogo Post Dar es Salaam.

Akizungumza na wanahabari, Sheikh Jalala amesema kuwa Wapalestina wamezagaaa duniani kwa kufukuzwa katika nchi yao na kuishi kwa mateso ambapo amesema kuwa wao kama Waislam hawawezi kukubali uvamizi kama huu kwa watu ambao hawana hatia hivyo wanaomba vyombo vinavyohusika vikiwemo vile vya umoja wa mataifa kuhakikisha wanarudisha amani kama iliyopo Tanzania kwani uwezo wa kufanya hivyo upo.

 

Ameeleza kuwa kwa mtu ambaye anatambua historia ya nchi hiyo ya Palestina na mambo yanayopitia ni dhuluma, ukandamizaji na mateso makubwa jambo ambalo halifai kunyamaziwa, huku akisema kuwa ni ukweli kwamba mambo ya Palestina ni ya Wapalestina ila kwa sasa Palestina haipo mikononi mwa Wapalestina jambo ambalo linawapa nguvu wao kuinuka na kupiga kelele juu ya wanadamu hao wanaoteseka bila hatia.

 Palestina

Itakumbukwa kuwa mgogoro wa nchi hizo mbili kati ya Israel na Palestina umekuwa wa muda mrefu huku ukisahaulika ambapo wananchi wa Palestina wamekuwa wakikumbana na mateso makubwa kutoka kwa majeshi ya Israel na hata wengine kuikimbia nchi hiyo kutokana na mateso hayo jambo ambalo limekuwa likiwanyanyua vinywa viongozi wa dini mbalimbali akiwemo Sheikh Jalala kulaani mateso hayo yanayoendelea nchini humo.

(PICHA NA STORI; EXAUD MTEIMSAKA)

Isikilize audio ya taarifa hii hapa chini;

Leave A Reply