The House of Favourite Newspapers

Siku ya kwanza Nisha Kukutana na ‘Serengeti Boy’ Wake Ilikuwa Hivi

0
Salma Jabu ‘Nisha’ na seerengeti Boy wake.

IMEFICHUKA! Staa wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amemfungukia mpenzi wake mpya anayejulikana kwa jina moja la Mino kuwa alianza uhusiano naye wa kimapenzi tangu Sikukuu ya Wapendanao (Valentine Day) lakini aliamua kufanya siri ili aendelee kujiridhisha kama ana sifa zote za kuwa mume bora.

 

Kwa kipindi kirefu kulikuwa na madai kuwa mwanadada huyo anabanjuka na ‘serengeti boi’ huyo lakini alikanusha vikali hadi siku chache zilizopita alipoamua kumtangaza hadharani.

 

“Mino nilianzana naye tangu mwaka jana siku ya Valentine, lakini sikupenda kukurupuka kumtambulisha kwa mashabiki wangu. Baada ya kugundua ni mwanaume wa tofauti na mwenye mapenzi ya kweli kwangu siyo kwa sababu ya kitu f’lan nikaamua niweke wazi na nyumbani kwetu nimeshaenda kumtambulisha wanamjua, bado kwenda kwao rasmi japo tayari wananijua,”alisema

 

Na Mayasa Mariwata | IJUMAA

Leave A Reply