The House of Favourite Newspapers

Snura: Faiza Anatafuta Pa Kutokea

Snura Mushi

MWANAMUZIKI Snura Mushi ameibuka na kusema kuwa pamoja na msanii mwenzake Faiza Ally kumtukana mitandaoni kwa kutumia kazi yake ya muziki lakini atakuwa amepata funzo kwa yale aliyomwambia kwani hatarudia tena kile alichokifanya cha kuweka video ya kujifungua mtandaoni na anachoona yeye Faiza anatafuta pa kutokea.

Msanii mwenzake Faiza Ally.

Akiongea na Risasi Jumamosi, Snura alisema kuwa kwanza yeye kwenye nyimbo zake haamasishi ngono kama yeye anavyofikiria bali anafanya muziki ambao ni asili ya Kitanzania kwani hata ngoma za asili watu wanakata mauno.

 

“Ninachojua mimi huyo anatafuta pa kutokea tu, nyimbo zangu mimi kamwe hazihamasishi ngono hizo ni fikra zake tu siwezi kumzuia, ninachokifanya ni kuonesha uhalisia wa Kitanzania kama zilivyo ngoma zetu,” alisema Snura.
Stori na Mwandishi Wetu

Comments are closed.