The House of Favourite Newspapers

Spika Ayaona Makontena ya Mchanga Yaliyozuiliwa Bandarini

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Job Ndugai,  leo ametembelea bandari ya Dar es Salaam na kujionea makontena yaliyotaka kusafirishwa nje ya nchi yakiwa na mchanga uliotoka katika migodi mbalimbali inayochimba dhahabu nchini.

Viongozi wa Bandarini wakimfafanulia jamboNdugai.

Ndugai ameyaona makontena 256 yaliyokuwa njiani kusafirishwa kwenda nje ya nchi siku chache baada ya Rais Magufuli kufanya ziara ya kushtukiza bandarini hapo.

Ndugai akipatiwa ufafanuzi juu ya makontena yaliyokamatwa.

Baada ya ziara hiyo, Ndugai alisema aliambatana na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ili kupata ufafanuzi wa kina kutoka kwa viongozi wanaohusika na masuala ya madini kuhusu makontena hayo ili bunge kama chombo cha kushauri serikali lichukue hatua mara tu kikao cha Bunge la Bajeti kitakapoanza.

Baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini walioambatana na Spika.
Ndugai akijionea makontena yenye mchanga wa dhahabu.
Spika Ndugai akizungumza jambo mara baada ya kuyaona makontena hayo.

NA DENIS MTIMA/GPL

Comments are closed.