Starline Films Mkombozi Wa Video Na Audio Bora
KAMPUNI ya Starline Films ambayo inatarajiwa kuwa mkombozi wanamuziki, wasanii wa filamu, waandaaji matangazo na wengineo kwa kazi za video na audio bora baada ya kuzinduliwa kampuni hiyo iliyopo Mikocheni B, jijini Dar.
Uzinduzi huo ulifanyika Ijumaa iliyopita ambapo Mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo.
Katika hafla ya uzinduzi huo wasanii wa filamu, waandaaji na wanamuziki walihudhuria.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.