The House of Favourite Newspapers

Taasisi ya Wananchi Wazalendo Tanzania Yatoa Elimu kwa Kutumia Michezo

0
Mgeni rasmi katika tamasha hilo, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wananchi Wazalendo Tanzania (TWWT) na Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kipolisi ya Kariakoo Dkt. Ezekiel Kyogo (wa tatu kutoka kushoto mwenye suti) wakiwa wamesimama ulipokuwa ukiimbwa wimbo wa taifa kabla ya mechi kati ya Polisi Chanika na Chanika Combine kuanza.

 

TAASISI ya Wananchi Wazalendo Tanzania (TWWT) imetoa elimu ya uzalendo kwa kutumia michezo katika tamasha lililofanyika Uwanja wa Kituo cha Wilaya ya Kipolisi ya Chanika jijini Dar.

Tamasha hilo lililokusanya maelfu ya wahudhuriaji lilianza na maandamano ya wananchi waliokuwa wakiimba nyimbo za kizalendo na kupambwa na burudani mbalimbali ikiwemo vigoma, matarumbeta na kumaliziwa na fainali ya mpira wa miguu kati ya timu ya Polisi Chanika na vijana wa Chanika Combine.

Mgeni rasmi akiwakagua wachezaji.

Katika fainali hiyo iliyokusanya maelfu ya watazamaji timu ya Chanika Combine inayoundwa na vijana wa maeneo hayo ndiyo walioibuka na kombe hilo sambamba na jezi mpya. Kabla ya mechi hiyo kulikuwa na maneno ya uhamasishaji uzalendo wa taifa la Tanzania yaliongozwa mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wananchi Wazalendo Tanzania (TWWT), Dkt. Ezekiel Kyogo ambaye pia ni Mkuu wa Upelelezi OC-CID wa Wilaya ya Kipolisi ya Kariakoo.

Umati wa mashabiki ukishuhudia wachezaji wakitifuana, Polisi Chanika waliovaa jezi za bluu na Chanika Combine nyeupe.

 

 

Katika tamasha hilo wananchi kwanza walifundishwa umuhimu wa kuipenda na kuijenga nchi yao kuaswa kutokubali kuisaliti kwa namna yeyote ile. Dkt. Kyogo amesema unakuta kuna mtu mwingine kwa kukosa uzalendo anasambaza mitandaoni picha au video zinazodhalilisha taifa.

Amandus Jordan ambaye ni Mwakilishi wa Taasisi ya Wananchi Wazalendo Tanzania kutoka Diaspora aishie Canada ambaye amerudi hapa nchini kwa ajili ya tamasha hili akizungumza na Global Tv baada ya kuhamasisha uzalendo kwa wananchi waliojitokeza.

 

 

Wananchi hao pia walielimishwa juu ya  kuacha uharifu na madhara ya matumizi ya dawa za kulevya na aina nyingine za vilevi haramu vinavyokatazwa na serikali ambavyo vimeshaharibu sana nguvu kazi ya taifa. Akizungumza kwenye umati huo Dkt. Kyogo alisema;

Katibu Mkuu wa Wanamuziki nchini, Stellah Joel na mumewe Dkt. Frank Richard wakizungumza na Global Tv baada ya kuhamasisha uzalendo kwenye tamasha hilo.

 

 

“Ndugu wananchi naomba tumuunge mkono Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan ambaye anaupinga mwingi kwa kuleta maendeleo ya kazi na kudumisha amani na utulivu.

Chanika Combine wakikabidhiwa kombe lao na mgeni rasmi, kushoto ni mke wa mgeni rasmi, Grace Sangija.

 

 

“Tusipokuwa wazalendo ni ngumu kuendelea kuwa na amani hivyo basi tukiwa wazalendo na nchi yetu tumuunge mkono Rais wetu Mama Samia Suluhu, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camilius Wambura, RPC wetu wa Kanda Maalum wa Dar es Salaam Murilo Jumanne na RPC wa mkoa wa Kipolisi wa Ilala tulipo hivi sasa, Kamishna Msaidizi, Debora Magilingimba”. Alimaliza kusema Dkt. Kyogo.                                                                                                                                                              HABARI/PICHA: NA RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY /GPL 

Leave A Reply