TAMISEMI Yatangaza Nafasi za Ajira kwenye Kada za Afya na Ualimu
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya TAMISEMI imetangaza nafasi za Ajira kwa Walimu na Madaktari ambalo utekelezaji wake wa maombi umeanza tangu jana Aprili 20 hadi Mei 4, 2022.
TAMISEMI imetoa maelekezo kuwa waombaji wa kada ya Ualimu ni kwa wale waliomaliza Vyuo kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2021 katika ngazi ya Cheti, Astashahada na Shahada.