The House of Favourite Newspapers

Tanzania Yashuka Nafasi 33 Viwango Fifa

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania.

 

TANZANIA imezidi kuporomoka katika viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ambapo hivi sasa inashika nafasi ya 147 kutoka 142 ya mwezi Oktoba.

 

Jana Alhamisi, Fifa ilitoa viwango hivyo ambapo inaonyesha ndani ya miezi mitano kuanzia Julai, mwaka huu, Tanzania imeshuka kwa jumla ya nafasi 33.

Ikumbukwe kuwa, kwa siku za hivi karibuni, Tanzania ilifanya vizuri kwenye viwango vya Juni baada ya kushika nafasi ya 114 kutoka nafasi ya 139 ya mwezi Mei. Baada ya hapo, Julai ikashika nafasi ya 120, Agosti 125, Septemba 136, Oktoba 142 na sasa Novemba ni 147.

 

Kushuka huko kwa Tanzania kuna­tokana na Novemba, mwaka huu, Taifa Stars kutoka sare ya bao 1-1 na Benin katika mchezo wa kirafiki uli­opigwa kwenye Uwanja wa l’Amitie, Benin.

 

Katika 10 Bora ya duniani, Ujeru­mani inaongoza ikifuatiwa na Brazil, Ureno, Argentina, Ubelgiji, Hispania, Poland, Uswisi, Ufaransa na Chile.

Comments are closed.