TANZIA: MAZISHI YA MPIGA PIGA ATHUMANI HAMISI KESHO
MWILI wa aliyekuwa mpigapicha wa magazeti ya serikali (TSN), Athumani Hamisi Msengi, unatarajiwa kuzikwa kesho Januari 5 mchana katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam. Mipango ya mazishi hayo inafanyika nyumbani kwa marehemu Sinza-Madukani, Mtaa wa Weruweru, Nyumba namba 26.
Marehemu amefariki asubuhi leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikofikishwa kwa matibabu baada ya kuzidiwa ghafla usiku akiwa nyumbani kwake.
Kampuni ya Global Group tunatoa pole kwa wote wanaohusika na msiba huu, tukimtakia marehemu mapumziko ya amani milele.
Comments are closed.