The House of Favourite Newspapers

TANZIA: Mzazi Mwenziye na Shilole Afariki Dunia

MZAZI mwenziye na  Staa wa miondoko ya mduara, Zuwena Mohammed , aliyejulikana kwa jina la Makala Elia Joseph, amefariki dunia leo Jumanne, Juni 5, 2018 nyumbani kwao Wilayani Igunga mkoani Tabora alikokuwa akiishi.

 

Akizungumza na www.globalpublishers.co.tz, Shilole amethibitisha kutokea kwa msiba huo na kusema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa.

 

Shilole ameeleza kwamba  kesho ataanza safari kuelekea Wilayani Igunga kwa ajili ya kuungana na ndugu, marafiki na waombolezaji kwa ajili ya mazishi ya mzazi mwenzake huyo.

 

Shilole na Elias wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike aitwaye, Joyce Elias (ambaye ni mtoto mkubwa wa Shilole).

 

Global Publishers inawapa pole wafiwa wote wa familia hiyo kwa kipindi hiki kigumu.

“Pumzika kwa Amani Elias Makala, Amen!”

Comments are closed.