Tawia Yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani
Umoja wa Wajane Tanzania (TAWIA) leo umeadhimisha Siku ya Wajane Duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar ambapo hapa nchini ni maadhimisho ya mara ya pili.
Kwa mujibu wa TAWIA wajane ni wengi sana zaidi ya wagane ambapo taasisi yao ina jumla ya wajane 700 na wagane 20 na imejipanga kuanzisha kituo cha pamoja ambacho kitasaidia wajane kupata huduma za ushauri nasaha, msaada wa kisheria, uchumi na matibabu ili kupunguza kero wanazokutana nazo pindi wanapofiwa na wenza wao.
Aidha TAWIA imekemea vikali tabia ya wajane kunyanyaswa, pindi wanapofiwa na wenza wao kama kuitwa wachawi na kuhusishwa na vifo vya waume zao, kunyang’anywa mali, watoto na wengine kufukuzwa kwenye nyumba walizojenga na waume zao wakati wa uhai wao.
Hata hivyo Mkurugenzi wa TAWIA, Rose Sarwat ameiomba serikali na taasisi zingine kuwaunga mkono katika harakati hizo.
Zifuatazo ni picha za maadhimisho hayo;
Na Gabriel Ng’osha/GPL