TBBF Yatangaza Mashindano ya Mr. Tanzania na Mr. Photogenic
CHAMA cha Watunisha Misuli nchini (Tanzania Bodybuilding Federation -TBBF) imetangaza rasmi tarehe maalum ambayo itafanyika mashindano ya Mr.Tanzania, Style, Icon (Mr. Handsome na Mr. Photogenic, Desemba 16 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar, Katibu Mkuu wa TBBF, Francis Mapungilo, alisema kuwa pia mashindano hayo yatakuwa na ‘reality show’ kupitia televisheni ya Azam TV 2.
Katika kuelekea mashindano hayo kutakuwa na mchujo kuanzia Desemba 12 kwenye kambi maalum itakayokuwa imeandaliwa na kutakuwa na semina maalum kwa majaji wa mashindano ya kutunishamisuli (bodybuilding). Aidha ameeleza kuwa utaratibu utakaotumika katika upatikanaji wa tiketi utakuwa ni kwa njia ya mtandao na vituo maalum ambavyo vitatangazwa.
HABARI: DENIS MTIMA | GLOABAL PUBLISHERS