TECNO Yaanika Washindi wa “Vibe la Krismasi, TECNO Yatosha”
Wakati tulipokuwa kuikaribisha sikukuu za mwisho wa mwaka, hapa namaanisha Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya, Kampuni ya simu janja zinazopendwa zaidi Afrika Mashariki, TECNO ilitangaza washindi wa zawadi mbalimbali za promotion yao iliyobamba nchi nzima ya “Vibe la Krismasi, Tecno Yatosha”.
Katika promosheni hiyo, wateja ambao walinunua simu za TECNO katika msimu huu wa sikukuu walizawadiwa zawadi mbalimbali kubwa na za kutosha kutoka TECNO ikiwa desturi ya kampuni hiyo kurejesha fadhira kwa wateja wake kila mwisho wa mwaka.
Promosheni hiyo ilijumuisha mikoa ambayo ni pamoja na Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma, Tabora, Bukoba, Mtwara na Morogoro.
Washindi hao ambao ni Peter Mhina, Evelyne John, Ligibu Chande waliojishindia mashine za kufulia, Salome Shirima, Pendo Selemani na Leila ambao wanatokea Arusha, Mwanza na Dar es Salaam walijishindia majokofu, Safi Kaputa, Sophia Saulo na Vicent ambao wanatokea Dar es Salaam, Mbeya na Arusha, wao walijishindia microwave za umeme katika hiyo iliochezeshwa Desemba 17, 23 na 31, mwaka 2021.
Wateja wa TECNO walitakiwa kununua simu za POP Series, SPARK Series na CAMON Series na kuingia kwenye droo kisha kuibuka mshindi. Kufahamu zaidi juu ya promotion hii au kufahamu duka gani la kutembelea sahihi lenye promosheni wapigie kwenye namba zao 0744545254 au 0678035208.