The House of Favourite Newspapers

Tigo Pesa Wamwaga Zawadi Na Mamilioni Ya Pesa Kwa Mawakala Wake Wakishua

0
Afisa Mkuu wa Tigo Pesa Bi. Angelica Pesha.

Kampuni namba moja nchini kwa utoaji wa huduma za Kidigitali Tigo Tanzania kupitia Huduma yake ya mfumo wa pesa Kidigitali Tigo Pesa, imetoa zawadi kwa Mawakala wake Wakubwa na Wadogo kutoka Tanzania Bara na Visiwani ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha Kampeni yake iliyofanya vizuri ya WAKISHUA. Akizungumza Usiku wa tukio hili la kihistoria lililofanyika Jijini Dar Es Salaam Afisa Mkuu wa Tigo Pesa Bi. Angelica Pesha amesema;

Wakala mshindi wa Jumla Bi. Neema Swai wa pili kulia akikabidhiwa mfano wa hundi ya pesa aliyojishindia. Kulia ni Afisa Mkuu wa Tigo Pesa, Angelica Pesha wengine ni wageni wa heshima kwenye hafla hiyo.

“Tukio la leo ni kwa ajili ya Mawakala wetu wakubwa na wadogo wanaotusaidia kila siku ili kuweza kuwafikia wateja wetu na kuwapa huduma za Tigo Pesa, tumeona tujumuike nao kusheherekea mafanikio yetu ya mwaka 2022 sambamba na hayo tutatoa zawadi mbalimbali kwa mawakala wetu waliofanya vizuri , akiwemo Bi. Neema Swai atajipatia Milioni 15 akiwa kama wakala aliyefanya miamala mingi zaidi kwa mwaka 2022”

Sehemu ya wageni waalikwa wakishuhudia matukio kwenye hafla hiyo.

Wengine ni Said Khatibu Wakala kutoka Zanzibar ambaye ndiye mmoja wa wakala  aliyetoa huduma kwa mda mrefu zaidi na kwa mawanda mapana.

Wakala Waziri Omary kutoka Kibaha ambaye ni wakala aliyefanya vizuri katika kanda ya Pwani, na  Saba General Enterprises Limited ambaye huyu ni Wakala ambaye anafanya miamala kiufasaha yaani hana malalamiko ya wateja”. Alimalizia kusema Angelica.

Kwa upande wake Bi. Neema Swai mshindi wa milioni 15 kutoka TIGO PESA kama wakala aliyefanya miamala mingi zaidi, ameipongeza Kampuni ya Tigo kwa kuamua kuwakumbuka Mawakala wake kwa kuwazawadia zawadi mbalimbali na kuwakutanisha pamoja.

Leave A Reply