The House of Favourite Newspapers

Trump Aondoka Hospitali, Akazia Vita Dhidi ya Corona

0

RAIS  wa Marekani, Donald Trump ameruhusiwa kutoka kwenye hospitali ya kijeshi ya Walter Reed alikokuwa amelazwa kwa siku tatu akitibiwa ugonjwa wa COVID-19.

 

Baada ya kuwasili kwenye Ikulu ya Marekani, White House, Trump alivua barakoa yake kwa ajili ya kupiga picha na aliendelea kutembea bila barakoa wakati wafanyakazi wa ikulu walipomkaribia kumsalimia.

 

Mapema jana, rais huyo wa Marekani alitangaza kuwa ataondoka kwenye hospitali hiyo iliyoko Maryland, karibu na Washington D.C. Katika ukurasa wake wa Twitter, Trump aliweka ujumbe wa video akisema kwamba anajisikia vizuri sana.

 

”Nimeondoka kwenye hospitali ya Walter Reed, ni jambo la kipekee sana. Nimejifunza mengi kuhusu virusi vya corona. Na jambo moja la uhakika, usiviache viyatawale maisha yako, usiviogope, utavishinda. Tuna vifaa bora kabisa vya matibabu. Na sasa najisikia vizuri. Asanteni sana,” alisema Trump.

Leave A Reply